KUMBE MVUTA SIGARA NI BORA KULIKO ANAE KUNYWA SODA KILA SIKU KAMA MAJI KWAKE.
Unaependa kunywa soda? Soma hadi mwisho Utafiti uliofanywa na Muungano wa Waandishi wa Habari za Uchunguzi Tanzania (Investigative Journalists Union of Tanzania- IJUTA) pamoja na tafiti zilizofanywa na wataalamu waliobobea katika afya ya umma duniani,umebaini kuwa vinywaji baridi aina ya soda ni hatari kuliko utumiaji wa sigara inayosababisha maradhi ya kansa katika mwili wa binadamu.
IJUTA imebaini kuwa makampuni makubwa yanayotengeneza vinywaji baridi aina ya soda yanatumia mabilioni ya dola kila mwaka kujitangaza na kutoa misaada ya kijamii kutokana na mauzo yake, bila kutaja madhara ya vinywaji hivyo kwa binadamu. Kwamba matangazo hayo yanayogharimu mamilioni ya fedha ndiyo yanayokifanya kinywaji hicho kuwa maarufu zaidi duniani, licha ya kuwa na madhara makubwa katika mwili wa binadamu. Utafiti wa lIJUTA unaonyesha kuwa utamu wa kupindukia iliomo ndani ya soda unawapumbaza wanywaji ili wasisikie ladha kali ya asidi iliyomondani ya soda. IJUTA imegundua kuwa kiwango cha asidi kilichobadili ndani ya soda hakiwekwi wazi kwa walaji kwsababu ya kuhofia kuwa wakibaini wataacha kikutumia kinywaji hicho. Inaelezwa pia kuwa madini ya cola yaliyo ndani ya soda yana kilevi aina kafein kinachomteka mnywaji kuwa teja wa kinywaji hicho.
Utafiti uliofanywa nchini Marekani unaonyesha kuwa soda huwekewa 'fructose' (sukari) nyingi kupitia mfumo wa sirapu ambayo inaongoza kwa kusababisha magonjwa ya unene, kisukari, ugonjwa wa moyo na magonjwa mengine sugu yanayowakabili Wamarekani wengi hivi sasa na dunia kwa ujumla. Marekani imeshapiga marufuku matumizi ya soda kwa watoto wenye umri chini ya miaka 12.
Dk. Mercola, mtaalamu wa masuala ya lishe asilia na tiba Marekani, amekaririwa akieleza kuwa soda ni hatari kwa binadamu sawa na mtu anayevuta sigara au zaidi. Watumiaji soda wamekuwa wakinywa kiasi kikubwa cha kaboni, kafeini (dawa ya kulevya), sukari ya kupidukia na asidi kali ambayo huvuruga afya zao sana.
soda imepigwa marufuku kutumiwa na watoto walio na umri chini ya miaka 12 na walio shuleni katika baadhi ya mataifa ya Ulaya na Marekani, kutokana na madhara ya kiafya yanayosababishwa na kinywaji hicho. Huku bongo,soda ndio kinywaji cha watoto na wangonjwa daaha ni hatari sana.
Soda haina lishe ya aina yoyote zaidi ya maji na sukari. unywaji wa soda huongeza kiasi kikubwa cha madini joto.
Madhara ya soda ni makubwa kuliko ya uvutaji sigara. Ukiweza acha au punguza kunywa soda. Usiwape watoto soda,wafundishe kunywa juice za matunda asili.
N.B Kunywa maji au juice ya matunda asilia ni bora kuliko unywaji wa soda. Kuwa na nidhamu juu ya Afya yako leo ili ufurahie ukuu wa muumba wetu uwapo duniani
Penda sana kutumia chakula kama dawa na sio dawa kama chakula. Siku zote chakula ni dawa kuwa ni mwenye nidhamu kwa kile unacho weka kinywani mwako kama hakina faida yoyote kwenye mwili niheri ukaachana nacho kabisa.
|
0 comments: